• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Friday, 14 April 2017

    Msanii Harmonize kutoka WCB ndani ya Bongo wiki hii alitembelea (+254) Kenya na kufanya mahojiano na vyombo vya habari kadhaa.

    Harmonize ambaye ni msanii mkubwa ndani na nje ya Tanzania ,pia ndiye msanii wa kwanza kusainiwa na lebo ya muziki ya WCB,na amekuwa akiendelea kudondosha ngoma kali kila anapofanya ngoma zake,amesema siri pekee ya yeye kuendelea kufanya nyimbo nzuri na zenye ubora ni kutokana na kufuata nyayo za bosi wake “Diamond platnumz” ambaye amekuwa akifaya kazi kwa bidii kila wakati,ijapokuwa ndiye msanii mwenye mafanikio makubwa Tanzania.
    Aidha Harmonize anayemiliki tuzo ya Afrimma amezulu(+254) Kenya na kama ilivyo ada, "Mzazi Willy" Tuva alimkalisha Msetoni na kupiga naye story kadhaa,na alisisitiza kwa kusema tunavyoongea Diamond yupo South Africa kwa ajili ya kazi”
    Aliongeza kwa kusema“Kama Diamond ndiye msanii mwenye mafanikio makubwa Tanzania na hana time ya kujiachia,hiyo inanipa nguvu kuzidi kupambana na mimi,” na alihitimisha kwa kuwaomba mashabiki wa muziki wake kukaa macho kwenye mtandao wa wasafi.com kwani muda wowote kuna kitu kizuri kinakuja


    No comments:

    Post a Comment