• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Friday, 14 April 2017

    Rais Magufuli alaani mauaji ya askari polisi nane (8) Tanzania

    Rais John Pombe Magufuli wa Tanzania amepokea kwa mshtuko mauaji ya askari polisi nane waliouawa na watu wasiojulikana jioni siku ya tarehe 13/04/2017.
    Taarifa kwa vyombo vya habari na vyanzo mbalimbali zinaeleza kuwa askari hao walitoka kwenye mpango kazi wao wa kawaida,ndipo waliposhambuliwa na watu wasiojulikana kwa kupigwa risisa kwenye eneo la mpakani mwa wilaya ya Kibiti mkoani Pwani,ambapo walikuwa na usafiri wa gari.
    Rais Magufuli amelaani tendo hilo na matukio yote ya kuwashambulia polisi akisema wanafanya kazi kubwa ya kuwalinda raia,ametuma salamu za rambirambi kwa jamaa na marafiki walioguswa na vifo hivyo huku akiwataka raia wote kushirikiana katika kukomesha vitendo kama hivyo.
    ''Nimeshtushwa na kusikitishwa sana na vifo vya askari wetu 8 ambao wamepoteza maisha wakiwa wanalitumikia taifa, naungana na familia za marehemu wote, jeshi la polisi na Watanzania wote katika kipindi hiki kigumu cha huzuni na majonzi ya kuondokewa na vijana wetu shupavu,namuomba mungu atupe moyo wa subira ,uvumilivu na ustahimilivu'',alisema rais Magufuli



    No comments:

    Post a Comment