• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Friday, 14 April 2017

    Mh Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania atazindua hosteli za chuo kikuu cha Dar es salaam

    Mradi wa ujenzi wa Hosteli za Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam pamoja na mradi wa nyumba za wananchi Magomeni pale Magomeni Kota,utazinduliwa jumamosi hii.

    Miradi hiyo miwili itazinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli jumamosi hii,ambapo mradi wa hosteli hizo unakadiriwa kugharimu shilingi bilioni 10 zitakuwa na uwezo wa kumudu zaidi ya wanafunzi 3,840.

    Hizi zitakuwa hosteli za wananchi wa chini kabisa kama ambavyo Rais wetu amekuwa akieleza nia yake ya kuwasaidia wananchi wa chini,na mpango ni kufanya kila mwanachuo atakayekuwa akitumia hosteli hizo awe akilipa shilingi laki moja na elfu kumi tu kwa muhula mzima,ambacho ni kiwango cha chini ukulinganisha na kodi za hosteli zilizopo mitaani.

    Aidha kesho mara baada ya Uzunduzi huo, Rais Magufuli pia anatarajiwa kuweka jiwe la msingi katika Ujenzi wa nyumba za Magomeni kota.

    No comments:

    Post a Comment