• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Saturday, 15 April 2017

    Rapa Bill Nass awashauri Roma mkatoliki na wenzake.

     
    Kwenye kipindi cha “The Weekend Chart Show” jana 14 april 2017 kinachorushwa na Clouds TV msanii rapa Bill Nass ambaye anatamba na na ngoma kali inayokwenda kwa jina la” Mazoea” amemsihi Roma Mkatoliki na wenzie ambao walikumbwa na mkasa wa kutekwa.

    Bill Nass amewataka Roma na wenzie kuendelea na maisha kwa kufanya kazi ingawa hawatokuwa vizuri lakini kwa sababu wana uhai na ni wazima hicho pekee katika maisha yao wanapaswa kumshukuru Mungu.
    "Wanapaswa kumshukuru Mungu kwa kuwa wameendelea kuwa hai,hivyo waendelee kufanya kazi kwa moyo ule ule, natambua inakuwa ngumu kiasi hasa unapokuwa na kumbukumbu mbaya kichwani ile pressure haikupi mzuka wa kufanya kazi.Kwa mfano, mimi tu nikiwa hivyo mood za studio zinakata. Japo wao wanaweza kuwa zaidi ya hapo,kiujumla hizo ni changamoto,so, isiwafanye wakaishia hapo as long as wako hai na wazima."Bill Nass.

    No comments:

    Post a Comment