• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Friday, 14 April 2017

    Serikali yapiga marufuku kilimo cha mabondeni na kwenye vyanzo vya maji.

    Hayo yamesemwa na makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan baada ya kufanya ziara katika bwawa la Kuzalisha umeme la Mtera ili kuona utendaji kazi kwenye Bwawa hilo baada ya kumaliza ziara mkoani Iringa.
    Makamu wa Rais amesema uharibifu mkubwa unaondelea kwenye mito inayotiririsha maji kuelekea bwawa la Mtera ndio chanzo cha maji kuendelea kupungua mwaka hadi mwaka hivyo hatua za kukabiliana na hali hilo ni lazima zikuchuliwe ili kukokoa bwawa hilo kukauka.
    Amesisitiza kuwa kutokana umuhimu wa bwawa hili la Mtera,linalotuletea umeme mkubwa nchini ni muhimu wafanyakazi,wa bwawa hili wawe wazalendo na ili liendelee kuleta tija kwa nchi nzima kwa maendeleo ya viwanda na shughuli za uzalishaji kwa ujumla.
    Meneja wa Kituo cha Kufua Umeme cha Mtera Mhandisi “John Sikauki' alitoa taarifa ya hali ya uzalishaji Umeme kwenye kituo hicho kwa makamu wa Rais, amemueleza Makamu wa Rais kuwa hali ya mitambo ni nzuri ambapo mpango wa matengenezo katika kituo hicho Umefanyika.
    Meneja wa kituo alimuomba makamu wa rais mama Samia Suluhu,kuwa serikali iweke mkazo kwenye uhifadhi wa bonde la mto ruaha ambalo ni moja ya chanzo kikuu cha maji yanayonufaisha uzalishaji wa umeme.

    No comments:

    Post a Comment