• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Sunday, 30 April 2017

    Serengeti Boys yaendeleza ubabe kwenye michezo yake ya majaribio ya kimataifa.

    Timu ya taifa ya vijana ya Tanzania chini ya miaka 17 ‘Serengeti Boys’ imepata ushindi wa tatu mfululizo ikiwa ugenini amabpo imeweka kambi maalum kwa ajili ya maandalizi kujiandaa na mashindano ya AFCON kwa vijana chini ya miaka 17 itakayoanza mwezi Mei 14, 2017.


    Serengeti Boys wameifunga timu ya taifa ya vijana ya Cameroon kwa goli 1-0 lililofungwa na Ally Ng’anzi kipindi cha kwanza katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa ambao unakuwa ni mchezo wa tatu Serengeti kushinda mfululizo.


    Baada ya kumaliza kambi nchini Cameroon itaondoka na kuelekea moja kwa moja Gabon ambako zitafanyika fainali za michuano hiyo ya vijana itakayoshirikisha mataifa nane



    No comments:

    Post a Comment