• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Sunday, 30 April 2017

    Baada ya kumchapa Vladimir klitschko,sasa Anthony Joshua amtambia Tyson Fury na kuomba pambano.


    Saa chache tu baada ya kumalizika kwa pambano la ndondi lililoziteka hisia za wapenzi wengi wa ndondi duniani ambapo bondia wa Uingereza Anthony Joshua ameshinda kwa KO katika round ya 11 dhidi ya raia wa Ukraine Wladmir Klitschko, sasa ametaka pambano dhidi ya bingwa wa zamani wa uzito wa juu Mwingereza mwenzake Tyson Fury.


    Katika interview baada ya pambano dhidi ya Wladimir Klitschko lililopigwa katika Uwanja wa Wembley jijini London na kushinda kwa KO raundi ya 11, Joshua alimuomba Fury ambaye ni Mwingereza mwenzie wazichape:“Fury, Tyson Fury, uko wapi baby? Ni hiki unachotaka kuona? Nafurahia kupigana, napenda kupigana.

    "Tyson Fury", najua ulikuwa unaongea sana na unataka kurudi na kushindana – nataka kuwapa watu 90,000 nafasi ya kuangalia usiku mwingine wa boxing. Nataka kupigana na kila mtu, nafurahia hii sasa.”Anthony Joshua.
    Naye bondia bingwa wa zamani katika ngumi hizo za uzito wa juu Tyson Fury alimjibu Anthony Joshua kwa kupitia akaunti yake ya mtandao wa twitter baada ya kusikia tambo hizo akisema amekubali kupambana ambapo aliandika:“Anthony Joshua umekubaliwa. Tutaupa ulimwengu pambano kubwa katika miaka 500. Nitacheza na wewe.” Tyson Fury. 



    No comments:

    Post a Comment