• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Sunday, 30 April 2017

    Mbao FC yamng'oa yanga katika mbio za ubingwa FA Cup kwa goli 1-0.

    Jumapili ya leo ya tarehe 30 Aprili 2017 ni siku ya historia mpya kwa timu changa katika ligi kuu hapa Tanzania Bara maarufu kama VPL kwa klabu ya soka ya Mbao FC ambayo inashiriki kwa mara ya kwanza katika ligi hiyo kutoka jijini Mwanza imefuzu kucheza fainali ya FA Cup au maarufu kama Azam Sports Federation Cup kwa kuwang'oa mabingwa watetezi wa kombe hilo Yanga SC ya Dar es Salaam.
    Wakiwa wamepanda daraja kutoka ligi kuu Tanzania bara kwa mara ya kwanza, wameweza kufuzu kucheza fainali ya kwanza katika historia yao kwa kuifunga Yanga kwa goli 1-0 katika mchezo wa nusu fainali uliochezwa kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.Goli pekee la ushindi wa Mbao FC lilitokana na kujifunga kwa mlinzi wa kati wa Yanga Vicent Andrew katika dakika ya 27 ya kipindi cha kwanza wakati akiwa katika harakati za kuokoa mpira wa krosi uliopigwa na mchezaji Pius Buswita wa Mbao FC.
    Matokeo hayo yanaivua Yanga ubingwa wa FA Cup (Azam Sports Federation Cup) ubingwa ambao waliutwaa mwaka uliopita kwa kuifunga Azam kwenye mchezo wa fainali.Hivyo Mbao FC watakutana na Simba SC kwenye mchezo wa fainali, mechi ambayo Simba ndio wanatarajiwa kuwa wenyeji kwa sababu ndio walikuwa wa kwanza kufuzu kucheza fainali baada ya kuifunga Azam FC kwenye mchezo wa nusu fainali uliochezwa hapo jana kwenye uwanja wa taifa


    No comments:

    Post a Comment