• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Sunday, 30 April 2017

    Papa Francis ahimiza mjadala wa kimataifa juu ya mvutano kati ya Marekani na Korea kaskazini.

    Kiongozi wa kanisa Katoliki Papa Francis anapendekeza ufanyike mjadala wa kimataifa wa kuleta suluhu ya mvutano unaozidi kutokota kati ya Marekani na Korea kaskazini.Papa Francis amesisitiza kuwa migogoro wowote ni vyema ukiisha kwa njia ya meza ya mazungumzo.

    Amesema kwamba umoja wa mataifa unatakiwa kufanya kazi ya ziada kwenye hili,kwani hapo nyuma kidogo manoari za kimarekani zilitia nanga huko rasi ya korea.na ni kwa mara kadhaa Rais wa Marekani Donald Trump ameonesha kuishutumu Korea Kaskazini kwenye mpango wake wa nyuklia.  
    baraza la ulinzi la Umoja wa Mataifa lilikaa na kujadili mpango wa nyuklia wa Korea Kaskazini lakini baadae kidogo lilifanyika Jaribo la kombora la Korea Kaskazini ambalo halikufanikiwa.



    No comments:

    Post a Comment