• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Tuesday, 25 April 2017

    Nyambizi ya marekani yatia nanga huko pwani ya korea kaskazini.

    Nyambizi ya jeshi la Marekani imetia nanga huko pwani ya Korea Kusini huku ikihofiwa Korea Kaskazini kufanya jaribio jingine la kombora au silaha za nyuklia.


    Korea Kaskazini inaadhimisha miaka 85 tangu kuanzishwa kwa jeshi lake Jumanne.na kwakuwa hivi karibuni Marekani na Korea Kaskazini wamekuwa wakijibizana kwa kutoleana vitisho.hivyo bunge la Seneti nchini Marekani limealikwa kwenye kikao cha kupashwa habari kuhusu Korea Kaskazini siku ya Jumatano katika ikulu ya White House.


    Nyambizi ya USS Michigan hutumia nguvu za nyuklia na hubeba makombora aina ya 154 Tomahawk na wanajeshi 60 pamoja na meli nyambizi nyingine ndogo, Meli hiyo inatarajiwa kushiriki kwenye mazoezi ya kijeshi pamoja na kundi la meli zinazoongozwa na Carl Vinson, kundi ambalo lilitumwa eneo la Korea kuonyesha ubabe wa kijeshi wa Marekani.


    Pyongyang ilichukizwa sana na kutumwa kwa meli hiyo na imetishia kuizamisha kwa "shambulio moja kubwa" dhidi ya ilichosema ni uchokozi wa Marekani.Rais wa Marekani Donald Trump alisema mapema mwezi huu kwenye mahojiano ya runinga kwamba angetuma "kundi kubwa la meli zenye nguvu" na kwamba Marekani ina nyambizi ambazo "zina nguvu zaidi, nguvu zaidi kabisa kushinda meli hiyo (Carl Vinson) ya kubeba ndege"

    Aidha nchi ya China imeendelea kutilia mkazo suala la maongezi ya mezani kwanza.


    No comments:

    Post a Comment