• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Saturday, 29 April 2017

    Mzamiru yassin anyakua uchezaji bora kwa mwezi march 2017.

    Kiungo wa timu ya soka ya Simba ya Dar es salaam ,”Mzamiru Yassin” ametwaa tuzo ya mchezaji bora wa mwezi march 2017 ya timu ya Simba,ambapo Mwezi wa tatu Simba ilicheza michezo mitano ambayo ni mchezo dhidi ya Mbeya City kwenye ligi kuu, wakacheza na Madini Fc kwenye kombe la shirikisho. na mechi tatu za kirafiki dhidi ya “Polisi Dodoma, Chemba Kombaini, na Mererani Kombaini”

    Simba imekuwa na utaratibu wa kumchagua mchezaji yoyote ambae ameonyesha kiwango skizuri na kuisaidia timu kupata matokeo mazuri kwenye michezo yake na kumtunuku tuzo hiyo kama motisha na hamasa kwa wachezaji wake ili waweze kuwa na morali ya kujituma na kuonesha uwezo mzuri utakaokuwa na tija kwenye timu.

    Wachezaji wengine ambao wameshawahi kunyakua tuzo hiyo ni Abdi Banda ambaye alipata mwezi Februari, Laudit Mavugo mwezi wa Kwanza. Hii ni Mara ya pili kwa Mzamiru Yassin kushinda tuzo ya Mchezaji bora wa mwezi kwa timu ya Simba.  

    No comments:

    Post a Comment