• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Saturday, 29 April 2017

    Mkali wa miondoko ya Hiphop Tanzania Fid Q,awashauri haya bongo movie.


    Iile sakata la kuzuiwa kwa uuzwaji na usambazaji wa movie za nje ambazo zimetafsiriwa kwa lugha ya kiswahili,ambazo zimeonekana kuliangusha soko la filamu za kibongo limeendelea kushika chati kwani watu mashuhuri wameendelea kutoa ushauri na mitazamo yao juu ya jambo hilo.

    Mkali wa Hiphop Tanzania “Fareed Kubanda maarufu kama Fid Q” ametoa ushauri wake kupitia kipindi cha “leo Tena cha Clouds FM “ kilichorushwa siku ya tarehe 28 april 2017.

    Fid Q amesema “harakati ambazo zinafanywa na mastaa wa Bongo Movie ni nzuri na wanahitaji kusapotiwa juu ya hili ili malengo yafikiwe”.

    Fid Q amewashauri wasanii na wadau wa Bongo Movie kuwa kitu kimoja, na kufanya kazi kama team na kutoa kazi zao kwa mpangilio ili kuzifanya kazi hizo kufika mbali tofauti na kuwa kwa wiki wanatoa filamu 5 au 10 ambazo zitakosa mpangilio mzuri utakaopelekea kuzorota kwa tasnia hiyo.lakini amesisitiza wajaribu kukaa chini na serikali ili wapate sapoti na kuongeza uhalisia katika kazi zao



    No comments:

    Post a Comment