• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Saturday, 29 April 2017

    Mh Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania JPM apata mapokezi ya nguvu mkoani kilimanjaro.

    Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli amewasili mkoani Kilimanjaro kwa ziara ya siku tatu, ambapo anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika sherehe ya wafanyakazi ‘Mei Mosi’.

    Mh rais amewashukuru wananchi wa mkoa wa kilimanjaro kwa kujitokeza kwa wingi na kuonesha kuiamini serikali yake,amesisitiza mshikamano baina ya watanzania wote ili kuweza kusukuma gurudumu la maendeleo ya tanzania.

    Ameeleza kwa msisitizo kuwa maendeleo hayana vyama,”hakuna mtanzania anayekula vyama,na sababu ya kuja hapa ni kuweza kuungana na wananchi wa kilimanjaro na taifa katika kuibua na kuondoa changamoto zinazowakabili wanachi wa Tanzania kwa ujumla”asanteni sana,sana alimalizia mh Rais JPM.

    No comments:

    Post a Comment