• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Sunday, 9 April 2017

    Marekani yapeleka meli za kivita huko rasi ya Korea.














    Jeshi la Marekani limezielekeza meli zake za kivita zielekee karibu na rasi ya Korea,meli hizo zikiwa zimebeba silaha za kivita ni baada ya korea kaskazini Kufanya majaribio ya silaha zake kwa kuimarisha silaha zake za kinyukilia.
    Msimamizi wa kijeshi wa Marekani ukanda wa Pacific ameeleza kuwa kujiandaa huko kijeshi ni muhimu sana, Meli hizo zinajulikana kama ”The Carl Vinson Strike Group” zina meli moja kubwa ya kubeba ndege za kivita na meli nyingine za kawaida za kivita zikiambatana nayo.
    Msemaji wa jeshi la Marekani anaitazamia Korea Kaskazini kama tishio kubwa zaidi kwa usalama wa eneo la Pacific.

    Anasema ushahidi ni jinsi taifa hilo linavyofanya mazoezi ya zana za kinukilia kiholela.Meli hizo maalumu zinauwezo mkubwa katika kufanya mashambulizi na kujizuia na makombora ya maadui.

    No comments:

    Post a Comment