• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Tuesday, 4 April 2017

    Mama Salma Kikwete aapishwa rasmi leo bungeni.


    Spika wa bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania Job Ndugai leo amemuapisha mke wa rais mstaafu wa awamu ya nne wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete, Mh Salma Rashid Kikwete kuwa mbunge wa Bunge wa kuteuliwa
    Mh.Salma kikwete aliambatana na mumewe ambaye ni rais mstaafu wa awamu ya nne Mh Jakaya Mrisho Kikwete, ambapo uwepo wake ulizua shangwe na shamra shamra miongoni wa wabunge na kuweza kuonesha hisia zao waziwazi za kumkumbuka kwa uongozi wake uliomalizika.
    Leo hii Bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania limeanza kikao chake cha kwanza cha mkutano wa bajeti

    Mama Salma Kikwete kama anavyotambulika na walio wengi nchini ni mjumbe wa halmashauri kuu ya Chama cha Mapinduzi taifa{CCM}, lakini pia inatajwa kuwa ni miongoni mwa wanawake wenye ushawishi mkubwa kweye jamii,thamani ya mwanamke ilindwe kwa maslahi ya taifa.

    No comments:

    Post a Comment