• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Thursday, 13 April 2017

    Mafurushi ya mabilioni ya pesa yamekutwa kwenye nyumba moja huko Nigeria.













    Taarifa za toka kwenye vyombo vya usalama nchini Nigeria, imeeleza kufichuliwa zaidi ya dola milioni 40, iliyo kwenye sarafu ya pesa za Nigeria na ya kimataifa, baada ya msako wa ghafla kwenye nyumba moja mjini Lagos.
    Tume ya kupambana na uhalifu wa uchumi na kifedha (EFCC), imesema kuwa, ilipata “noti nyingi za Marekani, pouni ya Uingereza na nyingine za naira, kwenye mifuko iliyokuwa imefungwa barabara, ndani ya nyumba moja yenye vyumba vinne vya kulala.


    Inasema kwamba wapelelezi waliingia kwa nguvu ndani ya nyumba hiyo na kunasa dola milioni 43 nukta 4, Pauni Milioni 27 na laki 8 na Naira milioni 23 nukta 2, taslimu.
    Aida taarifa zinasema kuwa, baada ya kupekuwa zaidi mojawepo nya vyumba hivyo, walipata pesa zaidi ndani ya kabati la nguo,inasemekana kuwa fedha hizo zinaaminika kupatikana kupitia njia haramu.

    Tume ya EFCC, inasema kuwa, mfichuzi wa kashfa hiyo, aliwajulisha wapelelezi kuhusiana na mienendo iliyojaa shaka kuhusiana na mabegi yaliyokuwa yakiletwa na kutolewa kwenye nyumba hiyo mara kwa mara.
    Maelezo toka kwa mmoja wa majirani wa karibu na nyumba hiyo, amefichua kuwa,

     “Mwanamke mmoja amekuwa akionekana katika jumba hili mara kwa mara akiwa na mabegi yenye maandishi Ghana Must Go. Alikuwa akionekana mwenye uchovu, mavazi machafu na mwenye wasiwasi mwingi, lakini urembo wake haukuwa ukiendana na mavazi hayo, pengine kujifanya ili asitambuliwe.” alisema jirani huyo.
    Taarifa nyingine zinasema kuwa, maafisa wa usalama waliwahoji walinzi katika eneo hilo na wakasema kuwa hakuna mtu aliyekuwa akiishi katika jumba hilo.



    No comments:

    Post a Comment