• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Thursday, 27 April 2017

    KRC Genk ya Mbwana Samatta yatoa sare ya kwanza kwenye play off ,mchezo wao dhidi ya AS Eupen

    Kwenye Ligi Kuu yaUbelgiji KRC Genk inayochezewa na mchezaji machachari mtanzania “Mbwana Samatta” walikuwa ugenini kucheza mchezo wao wa 5 wa play off wa Ligi Kuu Ubelgiji dhidi ya wenyeji wao AS Eupen.

    KRC Genk wakiwa na rekodi nzuri ya kuwa timu pekee katika timu 12 zinazocheza game za play off kutofungwa katika mchezo hata mmoja wakiwa wameshinda michezo minne,ambapo april 26 /2017, KRC Genk wamejikuta wakilazimishwa sare ya kufungana kwa goli mojamoja(1-1) walipokuwa ugenini na kuwafanya kupata sare ya kwanza.


    AS Eupen licha ya kuwa nyumbani walifungwa goli la mapema kwenye dakika ya 20 ya mchezo,bao lililopachikwa na”Malinovsky” akipachika goli la kwanza la Genk lakini AS Eupen walisawazisha goli hilo dakika ya 51, katika michezo ya play off KRC Genk na AS Eupen ndio timu pekee ambazo hazijapoteza mchezo katika timu 12 kwenye kundi A na B.

    No comments:

    Post a Comment