• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Thursday, 27 April 2017

    JPM atoa onyo kwa watakaocheza na muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John Pombe Magufuli ametoa tahadhari kwa mtu yeyote yule atakayejaribu kuvunja muungano uliopo kati ya Tanganyika na Zanzibar, na kwa kushirikiana na mwenzake ambaye ni Rais wa Zanzibar Dr. Ali Mohamed Shein

    Kwa msisitizo ameomba wananchi wote kujua umuhimu na kuwa na moyo wa kuuenzi na kuulinda muungano wa nchi hizo mbili zinazokamilisha jamhuri ya muungano wa tanzania,ambapo onyo hilo amelitoa leo mjini Dodoma wakati wa maadhimisho ya miaka 53 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, yaliyofanyika mjini Dodoma.

    Lakini pia Rais Magufuli(JPM) amekiri kuwa anatambua kuwa licha ya mafanikio yaliyopatikana kwenye muungano huu, pia bado kuna changamoto mbalimbali zinazoukabili Muungano,hivyo kuulinda muungano kwa kutatua changamoto za muungano ni suala ambalo kwenye awamu yake litazingatiwa ili kuimarisha muungano na kutimiza ahadi alizozitoa kwa wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


    No comments:

    Post a Comment