• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Wednesday, 19 April 2017

    Jiji la Madrid lapambwa na shamra shamra za ushidi wa kishindo

    Michezo ya robo fainali ya ligi ya mabingwa barani Ulaya kwa mechi zilizochezwa jana april 18/04/2017, kwenye mechi za marudiano klabu mbili za jiji moja la “Madrid” huko hispania ziliweza kufuzu kuingia hatua ya nusu fainali ya ligi ya mabingwa barani Ulaya, inayojulikana sana kama;“UEFA Champions League”.

    "Atletico Madrid" ambayo ilipewa baraka za kuingia kwenye hatua ya nusu fainali na "Leicester City" ya Uingereza baada ya kumaliza mchezo wao kwa sare ya mojamoja(1-1), na kwakuwa Atletico ilipata ushindi wa bao 1-0 kwenye mchezo wao wa kwanza,hivyo sare yao ya jaja imeiwezesha Atletico kufuzu hatua inayofuata.



    Ambapo "Real Madrid" kwa upande wao ndani ya dk 90 za kawaida,walitanguliwa na "Bayern Munich" kwa goli 2-1,na baada ya kupewa muda wa ziada ndipo madrid walipofanya maajabu kwa kupiga goli tatu ndani ya dk 30 za nyongeza,ni hapo CR7 alipokamilisha Hat Trick na goli moja likifungwa na Marco Asensio,na mpaka kipenga cha kuhitimisha mchezo huo ubao ulisoma 4-2.

    Shangwe zililipuka kwa mashabiki wa timu hizi kote duniani hasa nyumbani jijini Madrid,na kwa sasa wanasubiri matokeo ya michezo itakayofuatia,ili kujua nani atakuwa na nani.








    No comments:

    Post a Comment