• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Saturday, 22 April 2017

    Diamond platnumz ametoa majibu kamili kwa wanaosema chibu perfume imekuja kwa gharama za juu


    Kwenye uzinduzi wa chibu perfume Meneja wa Diamond Platnumz, Sallam SK alitangaza bei ya Perfume ya Chibu itakavyouzwa kwenye maduka, baadhi ya watu wamesema kuwa bei hiyo ni kubwa sana,ndipo “Diamond Platnumzi” akaamua kufunguka kwa kusema haya;

    "Diamond anatambua kuwa ili kusonga mbele mtu anapaswa kujitoa katika kutengeneza kitu au bidhaa yenye ubora”,

    "pia amesema kwa sasa chibu perfume imeingia kwenye chupa ya ujazo wa ml100 kama bidhaa ya kuanzia lakini kwa baadae watatengeneza kwa vipimo tofautitofauti ili wadau mbalimbali wenye uzalendo na wanaoweza kusapoti kazi za wazalendo waweze kunufaika na huduma toka kwa wazalendo wenzao”.

    :"Amesisitiza vijana kuendelea kuwa wabunifu,serikali itoe mchango wake kwa kuwasapoti vijana wao na kuonesha njia kwa vijana wengine kuwa inawezekana,kufanya kitu na kuleta ushinadani kwenye masoko makubwa kidunia.

    "Aliongeza kwa kusema gharama za uzalishaji wa bidhaa hiyo ilikuwa juu,kutokana na ubora wa bidhaa ambayo inahitajika sokoni,na uhitaji wa kukamata soko la ushindani,na anatambua mchango wa wadau tofauti katika kufikia malengo,kama media zote,watanzania na anaamini huu ndio mwanzo na muendelezo wa kuanzishwa kwa bidhaa nyingine zitakazobuniwa na vijana wa kitanzania".

    No comments:

    Post a Comment