• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Sunday, 30 April 2017

    Bondia wa Uingereza Anthony Joshua ameendelea kuing'arisha rekodi yake ulingoni

    Kwenye pambano la masumbwi la usiku wa April 19 mashabiki wa mchezo huo walishuhudia mpigano wa kihistoria,ambapo Anthony Joshua alimwangusha Wladimir katika raundi ya tano,lakini mambo yalimgeukia kwenye raundi ya 6 ambapo nae aliangushwa kwa mara ya kwanza tangu alipoanza mchezo huo.

    Joshua alitumia vizuri nafasi kidogo aliyoipata katika hatua ya kuufikia ushindi,kwa kutupa ngumi za kushtukiza zilizompeleka chini mpinzani wake na raundi ya 11 ndipo pambano liliposimamishwa.

    Uwanja wa Wembley ulitawaliwa na shangwe pindi mwamuzi aliposema kuwa Wladimir Klitschko amezidiwa na hatoendelea na pambano,Hivyo AnthonyJoshua ambaye pamoja na umri wake wa miaka 27 na kushinda mechi zote 18 za awali alizocheza kwa ushindi wa KO,hivyo pambano la jana litajumuisha michezo 19 aliyoshinda na kuzidi kujiwekea rekodi ya ubora katika katika tasnia hiyo ya ndondi za uzani wa juu.

    No comments:

    Post a Comment