• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Friday, 21 April 2017

    Al shabab yawataka wazazi nchini somalia kutowapeleka watoto wao shule.

    Kundi la Al-Shabab latoa onyo kwa wazazi nchini Somalia, kwamba wasiwapeleke watoto wao katika shule na vyuo vikuu visivyokuwa vya Kiislamu.
    Kundi hilo limedai kwamba mfumo wa elimu wa magharibi unazorotesha maadili,msemaji wa kundi hilo “Ali Mohamoud Rage” ameonekana kwenye mkanda wa video, akisema mtu yeyote akijihusisha na elimu inayoeaneza mila na tamaduni za kigeni watakabiliana nae vilivyo.

    Hivi karibuni al-Shabab lilizindua mtaala wake wa elimu kwa lugha ya kiarabu,na kwa upande wa serikali ya Somali imelishutumu kundi hilo kwa kujaribu kuwanyima watoto wa Kisomali elimu bora huku wakiendelea kupandikiza itikadi yao inayosimamia mapigano na mauaji.


    No comments:

    Post a Comment