• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Friday, 28 April 2017

    Polisi DSM imetaja watuhumiwa wanaoshikiliwa juu ya tukio la vurugu za CUF.


    Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Simon Sirro amesema kuwa Jeshi hilo limewakamata watu saba katika tukio hilo na tayari Jalada limepelekwa kwa Wakili wa serikali kwa ajili ya kulisoma na kuandaa mashtaka ili wafikishwe Mahakamani.

    Amewaomba wote waliojijua kuwa wamehusika na kufanya,fujokwenye tukio la mkutano wa CUF,wajitokeze lakini amebainisha watu saba wameshakamatwa na taratibu zinaendelea kwa sasa,na jalada limefunguliwa na kupelekwa kwa mwana sheria ili sheria ifuate mkondo wake.

    Ametoa katazo kwa maandamano yasiyo ya msingi,na kama kuna makatazo ambayo yamewekewa,mipaka inatakiwa tuzingatia.

    Alimalizia kuwa oparesheni mbalimbali zinaendelea vizuri,dawa ya kulevya yanaendelea kukamatwa kwa waliojihusisha,kwani wamekamata wezi wa pikipiki na wameendelea kutoa ushirikiano kwa kusaidia kupatikana mtandao wao,lakini pia wameshakamata magari kadhaa pamoja na mmoja wa wamiliki wa gereji bubu ambayo imekuwa ikipokea magari yanayoibiwa.







    No comments:

    Post a Comment