• DON'T MISS

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****

    *****ADVERTISE HERE WITH US*****
    RABA CLASSIC

    Monday, 10 April 2017

    Kasi ya Singida united na maandalizi ya ligi kuu Tanzania bara.

    Timu ya Singida United baada ya kupanda ligi kuu imeendelea na jitihada za kujiimarisha,kwa kuendelea kufanya usajili utakaoleta tija na upinzani ligi kuu, baada ya kuwasajili wazimbambwe watatu Tafadzwa Kutinyu kutoka Chicken Inn, Elisha Muroiwa na Wisdom Mtasa wote kutoka Dynamos ya Zimbambwe sasa wako mbioni kufika Rwanda kwa ajili ya kumsajili Danny Usengimana mshambuliaji hatari wa Polisi ya Rwanda.
    Habari toka kwa mdau wa karibu zinaonesha kuwa Singida united wana nia ya kupata saini ya mchezaji,mshambuliaji wa Amavubi ya Rwanda Danny Usengimana, japo mpaka sasa Singida United hawajaweka wazi jambo hili.
    Danny Usengimana ni mchezaji hatari, katika msimu uliopita alitwaa tuzo ya mchezaji bora wa ligi ya Rwanda.Na hii sio mara ya kwanza kwa wachezaji kutoka Rwanda kuja kucheza Tanzania, Haruna Niyonzima ni miongoni mwa wachezaji kutoka Rwanda anayecheza ligi kuu ya Vodacom Tanzania.

    No comments:

    Post a Comment